MAJUKUMU YA KOCHA MPYA SIMBA

Klabu ya Simba imemtambulisha rasmi Mbrazili, Robertinho Oliviera kuwa Kocha wao Mkuu mpya kwa mkataba wa miaka miwili.

Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Mwenyekiti wa Klabu hiyo, Murtaza Mangungu amesema uzoefu wa Robertinho kwenye mashindano mbalimbali ndio sababu kubwa ya viongozi kumkabidhi jukumu hilo.

"Hakuna asiyejua alichokifanya katika timu mbalimbali alizofundisha na mfano mzuri tu ni kuifikisha hatua ya makundi Vipers kwa mara ya kwanza kwenye historia yao," amesema Mangungu.

Kuhusu hatma ya Juma Mgunda ndani ya kikosi hicho, Mangungu amesema asingependa kuweka wazi juu ya hilo ingawa mashabiki na wadau wanapaswa kutambua bado ni mwajiri wao na ataendelea na majukumu yake kama kawaida.

Post a Comment

Previous Post Next Post