LATRA YAPANDISHA NAULI ZA MWENDOKASI NA TAX MTANDAONI

Mamlaka ya Udhibiti wa usafiri Ardhini (Latra) imetangaza ongezeko la nauli za mabasi ya Mwendokasi jijini Dar es Salaam na zitakazoanza kutumika siku 14 zijazo kuanzia leo Jumanne Januari 3, 2023.

Akitangaza nauli hizo leo jijini Dodoma, Mkurugenzi Mkuu wa Latra Habibu Suluo amesema nauli hizo zimeongezeka kwa Sh100 kutoka nauli za zamani.

Mbali na nauli mpya za mabasi ya Mwendokasi, Suluo pia ametangaza nauli mpya elekezi kwa teksi mtandao, viwango vipya ambavyo viko katika makundi manne ya magari ya kubeba abiria sita, abiria wanne, pikipiki ya magurudumu matatu (bajaji) na ile ya magurudumu mawili.
Hata hivyo, Latra imepinga ombi la kuongeza nauli kwa wanafunzi na kubakia Sh200 iliyokuwepo.

Suluo amesema nauli ya mabasi ya Mwendokasi kwa njia kuu (truck route) ni Sh750 kutoka Sh600, njia ya mlisho (feeder router) ni Sh500 kutoka Sh400, njia ya mlisho na njia kuu (feeder +truck route) ni Sh900 kutoka 800 na njia ya kimara kwenda Kibaha ni Sh700 badala ya pendekezo la DART la Sh1,200.

Kwa upande wa nauli za teksi mtandao zinazobeba abiria wanne nauli itakuwa Sh3,000 hadi 4,000 kwa safari isiyozidi kilomita moja na kama kuna safari nyingine toka hapo nauli itaongezeka kwa Sh800 hadi 1,000 kwa kilomita moja na safari inapokutana na vikwazo kama foleni nauli ya ziada itaongezeka kwa Sh80 hadi Sh100 nauli kwa dakika.



Post a Comment

Previous Post Next Post