VIONGOZI WA EAC WAWATAKA WANAJESHI WA M23 KUONDOKA CONGO DRC HARAKA

Viongozi wa kikosi cha nchi za jumuiya ya Afrika Mashariki EAC wamelitaka kundi la waasi wa M23 kujiondoa katika maneo wanayoyadhibiti katika wilaya ya Rutshuru. 

Viongozi wa jeshi  la Kenya wanaohudumu nchini Kongo  chini ya EAC wamesema, kuondoka kwa M23 katika maeneo hayo ndiyo njia pekee ya kutekelezea makubaliano ya mkataba wa Angola na Nairobi. 

Kundi la M23 limekuwa likiendesha mashambulizi yake nchini mashariki mwa Kongo na kusababisha hali ya usalama kuwa tete, mauaji ya raia huku maelfu kuyakimbia makazi yao.

Kinshasa imekuwa ikiishutumu nchi jirani ya Rwanda kulifadhili silaha kundi hilo, hata hivyo Kigali imekuwa ikikanusha shutuma hizo.

Post a Comment

Previous Post Next Post